hadithi fupi....

                                                    nimejikwaa  



              
Scene 1
(akiwa sebureni na wazazi wake,mazoea alitazama simu yake ya kiganjani uku akitabasamu,alikua amehama kimawazo ,akihangaika kujibu kila ujumbe uliofika katika simu yake)
(Bi.masinde ambaye ndiye mama yake mazoea alikua amekasirishwa na tabia aliyokuwa akiionyesha mazoea…baada ya kumuita  kwa kipindi kirefu bila  ya kupata majibu yoyote .
Bi masinde::we mazoea!!!,
(mazoea akashituka  kama mtu aliyetoka usingizini,nakuanza kuwatazama wazazi wake kwa mshangao
Mazoea:naam baba.
Bi.masinde: siyo baba yako!!!, ni mimi ndiyo nakuita(kwa ukali),yani watoto wa siku hizi!!,
(bi masinde alivuta pumzi kidogo,ili aweze kuongea kwa utaratibu)
Bwana masinde:ngoja niwaache kidogo muongee
Bi masinde: mume wangu unaenda wapi?, ili swala hutakiwi kulitazama kwa jicho la upande kabisa!,sote tunahusika na hili swala
Bwana masinde:ninaelewa vizuri mke wangu ila kuna kitu kimetokea kazini inabidi nifike
(bwana masinde aliinuka kitini nakuondoka,bi masinde hakupendezwa na jibu la mume wake, akarudi kumtazama mazoea ,nakumkuta akitabasamu huku akiitazama simu yake ya kiganjani)
Bi masinde: mwana mwenye hekima humfurahisha babaye bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye,nimeamini!
(mazoea aliacha kutumia simu nakuieka pembeni,kisha akaanza kumtazama mama yake aliekuwa akitabasamu uku akimuangalia kwa jicho la udadisi,lililomfanya mazoea kujishitukia)
Bi masinde:mazoea unataka kuwa mzigo kwangu si ndio?
Mazoea:samahani mama!
Bi masinde:samahani ya nini?,
Mazoea: umeniita ..sikukusikia
Bi masinde:mwanangu mazoea,maisha ni kama msitu mkubwa,na ni kazi sana kujua vilivyo jificha ndani ya msitu ,bila kuwa mwenyeji wa msitu huo,na kama kila msitu,kuna kila aina ya hatari na pia kuna vizuri ndani yake,maua na matunda katika miti ya misituni uwa mazuri na yakuvutia ,uwavutia wanadamu pamoja na wadudu waumao na kudhuru,unanielewa mazoea?
Mazoea: (kwa kusita)..hapana mama?
Bi masinde: mwanamke mzuri asiye na akili ni sawasawa na pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,mwanangu upendo ni zawadi ya kwanza aliyotupa mungu wetu ,na upendo hauwezi thibitika bila ya kuonyeshwa mapenzi,lakini mapenzi ni kama maua mazuri yaliyopo msituni,sio tu vipepeo hupendezwa na maua bali hata nyuki na wadudu wakali,nimefurai umetambua aina nyingine ya upendo Lakini siwezi nikakuangalia ukijiingiza katika njia ya upotovu,juzi nimekuona tena ukiwa na Yule kijana,Yule bodaboda….alie tupeleka kanisani kipindi tuna amia katika huu mtaa,nimeona jinsi ulivyoukuwa ukiongea nae,nakuomba iwe mwanzo na mwisho,sitaki nikukute tena ,na uyaache mazoea na yule kijana…...
Mazoea: sawa mama nimekuelewa
(mazoea alijibu huku akijisikia aibu,mara simu ya mazoea ikaita,jina likatokea “jack”,
Bi masinde:anaitwa jack?
Mazoea: ndio
(bi masinde aliinuka na kuelekea chumbani kwake ambapo shughuli nyingine za nyumbani zikaendelea.)
Scene 2

(baada ya siku mbili kupita,jack alikuwa ana mawazo sana ,hakuwa tayari kuachana na mazoea,alikuwa kijiweni akifikiri chakufanya)
Selemani: (rafiki yake jacky)….oyo naona leo hauko sawa kabisa ,vipi au ndo mambo ya mama zuena tena
Jacky:mama zuena!!?, aah achana naye,mke wa mtu sumu aisee,yani tangia nikutane na mazoea ,mama zuena nimeshamsahau kabisa
Sele: duuh!,kile kigashi cha kilokole,daah we hatari,hadi pale umeshaingia?
Jacky:ah!,bado sijala,siunajua wale wanapenda mapenzi ya kweli,dah ila mkali
Sele:sasa mawazo ya nini tena?
Jacky: juzi sikaniambia anataka asome sijui,mara anaogopa,nimsubiri hadi ndoa,agh!! ,habari ya mapenzi basi,alafu bi mkubwa wake kagundua naona, maana alipita akanikazia macho kichizi.
Sele: aaah!.kwani asomi?,au ndo inshu ya mapenzi na shule na mambo ya bwana yesu hapendi,hahahaha !, sasa mbona  iyo inshu ndogo tu, mtoto muite geto,mwambie unaumwa akija tu,hucheleweshi, baada ya apo atajijua yeye na yesu wake.
(jacky akatulia kimya kidogo,ghafala akatokea bwana masinde ambaye alikuwa akitoka kazini na kutaka usafiri wa bodaboda hadi kwake,bwana masinde alizoea kutumia usafiri wa jacky kutokana na uendeshaji mzuri wa jacky., .jacky aliona ndio kapata fursa ya kumuona mazoea,na safari ikaanza hadi nyumbani)
Bwana masinde: (alipofika nyumbani,)…mama mazoea!!,mama mazoea!!.
(Aliita bila mafanikio,)……..mazoea!!,mazoea!!
Mazoea: abee baba
Bwana masinde:njoo haraka,ulikuwa wapi ,mi naita muda wote?
Mazoea:nilikuwa najiandaa kuendaa kanisani
(mazoea alishitushwa baada yakumuona jacky aliyekuwa akimtazama kwa makini sana,kama mtu anaetoa ishara ya ujumbe usoni)
Bwana masinde: yani leo hukuenda  mitha ya asubuhi na mama yako?...eeh!!,haya yukwapi mama yako,emu ingiza hii mizigo ndani
Mazoea:sawa baba,mama ametoka,hajaniaga
Bwana masinde; sasa atakua ameelekea wapi,nilitaka niongee nae ndo niondoke, na nampigia hapa hapatikani,
(baada ya mazoea kupeleka mizigo ya baba yake ndani,anatoka tena nje)
Bwana masinde: sasa kijana naomba umpeleke mwanangu kanisani,apa mimi itabidi nimsubiri uyu mwanamke, embu nipe namba yako,napenda sana huduma yako na una heshima kwakweli
(jacky alitabasamu na kumpatia namba yake mzee masinde,akampakia mazoea,ambaye alikua akionyesha sura ya wasiwasi,baada ya jacky kuwasha pikipiki alielekea moja kwa moja hadi nyumbani kwake,wakati wote mazoea alikua akilalamika kuwa anahitaji kuenda kanisani)
Jacky:mazoea mbona umebadilika sana,ninakupenda, siwezi ishi bila yako mazoea,
Mazoea:hata mimi ninakupenda jacky lakini….
Jacky : lakini nini mazoea (uku akimvuta mkono mazoea waingie ndani)
Mazoea:jacky!!!.hapana ndani siingii,tuongelee hapahapa na unipeleke kanisani
Jacky:kwanin usiingie mazoea,mara moja tu
(baada ya jacky kumlazimisha sana mazoea hatimaye wanaingia ndani ambako mazoea anashawishika kufanya tendo la kimapenzi kwa mara ya kwanza,)

                                                                        Scene 3

Baada ya wiki moja
Jacky:jomba mbona kimya,sioni kitu mezani
Alfred:asee uyu mtoto ulimtoa wapi anaonekana sio mzoefu wa mambo kabisa
Jacky:aah gashi mmoja wakilokole,vipi sasa iyo video ushairusha au?,hujanipa mkwanja,sikusomi yani
Alfred:usikonde babu,muda wowote ngoma iko hewani,mzigo nakutumia sasa ivi
(jacky alichukua rekod ya video ya tendo la faragha  alilokuwa akifanya na mazoea na sasa video ilisambaa mitandaoni baada ya jacky kuiuza kwa wasambazaji  wa video za ngono,magazeti ya udaku yalichapisha nakala yakiwa na kichwa cha habari “AIBU TUPU”,video ilisambaa na kila mtu akajua,ilikua ni aibu kubwa katika familia ya mzee masinde,)
Bwana masinde: iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu,lakini mwisho wake ni njia ya mauti,hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni.
(kanisani pia na shuleni kwa mazoea habari ilisambaa,mazoea alifadhaika sana na kujiona asiye na thamani katika jamii,alirudi kwa mama na baba yake akilia baada ya kutoroka kwa kipindi cha siku mbili kutokana na aibu iliyojaa katika nafsi yake,na mama yake alikua wa kwanza kutamka neno baada ya kimya cha muda mrefu
Mama masinde:nimekusamehe mwanangu( huku akilia alimfuata mwanae na kumkumbatia.





                                                        mwisho
….



Maoni